| Home | Bookmark | Tell | Active petitions in over 75 countries | World Times |
TUPATIENI 'STIEGLERS GORGE' |
81 Signatures |
Published by Edward chacha on Oct 30, 2006
Category: National Affairs
Region: Tanzania
Target: Tanzania citizens
Web site: http://www.bongotz.com
Background (Preamble):
Lengo letu ni kukusanya sahihi zipatazo milioni moja na kuziwakilisha kwa Rais Kikwete tukiitaka serikali iwekeze kwenye mradi wa Stieglers Gorge, uliopo kwenye bonde la mto Rufiji wenye uwezo wa kuzalisha umeme wa Megawatt 2100 [mwingi wa kutosha na hata mwingine kubaki na kuuzwa nje ya nchi] ili tuweze kuondokana kabisa na tatizo hili la kukatikiwa na umeme, tatizo ambalo ni aibu kubwa kwa taifa letu.
Petition:
Stieglers Gorge ni nini hasa?--Stieglers Gorge ni mpalio mwembaba unaopatikana kwenye bonde la mto Rufiji, kilomita 374 toka jijini Dar es salaam. Kwa utafiti uliowahi kufanyika mwishoni mwa miaka ya sabini na mwanzoni mwa miaka ya themanini [ 1978-1980] kwa ushirikiano wa RUBADA [Rufiji Basin Development Authority] na M/s Norplan/Hafslund, ilionekana kwamba mradi wa Stieglers Gorge una uwezo mkubwa wa kuzalisha umeme mwingi kwa njia ya maji [Hdro-power] zaidi ya umeme ambao Tanzania ilikuwa ikihitaji katika miaka hiyo.
Matokeo ya utafiti huo pia yalionyesha kwamba, mpalio wa Stieglers una uwezo wa kuhimili mitambo mitatu mikubwa ya kuzalisha umeme [3 power stations]. Mtambo 'A' wenye uwezo wa kuzalisha megawati mia nne (400MW) ambao ungefungwa upande wa kaskazini mwa bwawa [dam]. Mtambo 'B' wenye uwezo wa kuzalisha megawati mia nane (800MW) ambao ungefungwa upande wa chini ya bwawa, na mtambo 'C' wenye uwezo wa kuzalisha megawati mia tisa (900MW) ambao ungefungwa upande wa kusini mwa bwawa. Jumla megawati elfu mbili mia moja [2100MW].
Matokeo ya utafiti huo pia yalionyesha kwamba, mpalio wa Stieglers una uwezo wa kuhimili mitambo mitatu mikubwa ya kuzalisha umeme [3 power stations]. Mtambo 'A' wenye uwezo wa kuzalisha megawati mia nne (400MW) ambao ungefungwa upande wa kaskazini mwa bwawa [dam]. Mtambo 'B' wenye uwezo wa kuzalisha megawati mia nane (800MW) ambao ungefungwa upande wa chini ya bwawa, na mtambo 'C' wenye uwezo wa kuzalisha megawati mia tisa (900MW) ambao ungefungwa upande wa kusini mwa bwawa. Jumla megawati elfu mbili mia moja [2100MW].
The TUPATIENI 'STIEGLERS GORGE' petition to Tanzania citizens was written by Edward chacha and is hosted free of charge at GoPetition.
Promote this petition with a popular social bookmarking service [?]:
















